Arsenal Charii!, Yabugizwa 4-1 na Chelsea Emirates.


Timu ya Arsenal imepewa kipigo cha nguvu ambacho hawakukitegemea toka kwa Chelsea kwenye uwanja wao wa Emirates baada ya kukubali kubugia magoli 4-1.
Timu zote mbili ziliingia uwanjani leo zikiwa na majeraha ya kutupwa nje ya kombe la mabingwa wa ulaya katikati ya wiki iliyopita.

Uzoefu katika soka ulidhirika kuwa ni muhimu sana baada ya vijana wa Arsene Wenger kutawala dakika zote 45 za kipindi cha kwanza lakini mwishoni mwa kipindi hicho Arsenal ilikuwa tayari imeishabugia mabao mawili.

Chelsea waliwashtua wenyeji wao kwa mabao mawili ya haraka haraka katika kipindi cha kwanza kupitia kwa Alex na Kolo Toure na kuifanya Chelsea iende mapumziko ikiwa kifua mbele kwa mabao 2-0.

Dakika nne baada ya kuanza kwa kipindi cha pili jahazi la Arsenal lilizidi kuzama baada ya beki wake Kolo Toure kuizawadia Chelsea goli la tatu katika dakika ya 49 kwa kuuzamisha nyavuni kwake mpira wa krosi iliyochongwa na Asheley Cole.

Nicklas Bendtner aliifungia Arsenal goli la kufutia machozi katika dakika ya 70 kabla ya Malouda kuhitimisha karamu ya magoli ya Chelsea katika dakika ya 86.

Chelsea kwa ushindi wa leo imejihakikishia nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ya Uingereza.

Katika mechi nyingine iliyochezwa leo, Manchester United imekinyakua tena kiti chake cha uongozi wa ligi baada ya kuwagaragaza mahasimu wao Manchester City kwa mabao 2-0.



0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2009 Bloggerized by : CTU | Inspired By ReedzSolution : ReedzSolution