Baada ya Kumtosa Chris Brown, Rihanna Amrudia Mpenzi wake wa Utotoni.


Rihanna mwenye umri wa miaka 21 alikuwa akitoka na Negus Sealy ambaye sasa ana umri wa miaka 24 kabla hajamtosa alipokuwa maarufu.

Taarifa za udaku zilisema kwamba wapenzi hao wa zamani wameamua kuyakumbukia mapenzi yao baada ya Rihanna kuachana na Chris Brown ambaye alimshambulia.

Sealy ametajwa kama ndiye mtu anayemliwaza Rihana na kuwa bega la kulilia la Rihanna baada ya kuvunjwa moyo wake na Chris Brown ambaye alimshambulia na kumjeruhi usoni.

Chanzo hicho cha udaku kililiambia gazeti la News of the World la Uingereza: 'Sealy ndio sehemu ya kujiliwaza ya Rihanna, ni kijana mtanashati, mwenye busara na mpole".

"Mademu wote wanamzimia na kumuita 'mtaalamu wa mapenzi' alikuwa akionekana na Rihanna kabla Rihanna hajawa maarufu".

Wapenzi hao walionekana wakila raha katika ufukwe mmoja katika kisiwa cha Barbados ambapo Rihanna alikuwa amevaa bikini nyeusi na kofia vilivyomkaa vilivyo na kumfanya aonekane 'Hot'.

Rihanna inasemekana kwa jinsi alivyojitosa mzima mzima kwa Sealy huwaambia rafiki zake na familia yake kwamba mapenzi yake na Chris Brown yatabakia kuwa historia.

Chris Brown alipandishwa kizimbani jijini Los Angeles mwezi na alikataa madai ya kufanya shambulizi, akipatikana na hatia anaweza akapewa kifungo cha hadi miaka mitano jela.



0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2009 Bloggerized by : CTU | Inspired By ReedzSolution : ReedzSolution